Skip to main content

How to(Jinsi ya)...kuwa Chini ya "Mumeo"....


....imekuwa kawaida kwa Wanandoa Wake kwa Wame kutafuta "jinsi ya" kufanya mambo mbali mbali ili kuifanya Ndoa kusimama Imara na kuepusha misuko-suko ya kihisia na hivyo kupelekea Ndoa kuwa Ndoano na pengine kuharibika.


Hii kuwa "chini ya Mumeo" hata mie siijui na vyovyote ilivyo kamwe sitokubali kuwa "Chini" ya  Mtu yeyote achilia mbali Mwanaume ila nitakuambia ninachokijua ambacho huenda ni tofauti lakini bado kinamrudishia Mwanaume hali ya kujihisi/sikia kuwa anaheshimika/heshimiwa na Mkwe.



Tatizo kubwa linalofanya Wanawake kukumbushwa au lazimishwa na Jamii kuwa ni LAZIMA wawe chini ya Wanaume (asiwe na Sauti) pale wanapoamua kufunga Ndoa ni kutokana na Imani kuwa Mwanamke anaposimama na "kujitetea" na/au kum-challenge Mwanaume basi huesabika kuwa hana Adabu, hana Heshima kwa Mwanaume husika.




Ukweli ni kuwa unapokuwa kwenye Ndoa ya "ndio Bwana"  kwamba kila anachokisema Mwanaume wewe unakubali tu....huondoa Changamoto na hivyo kufanya Ndoa kuwa a bit "boring" na ni wazi kuwa hautofurahia Ndoa hiyo kwa sababu hautokuwa na Sauti,...Ndoa inaendeshwa na Mtu mmoja, kwamba kuna maamuzi yatakuwa yakifanywa na Mumeo ambayo wewe hupendezwi nayo lakini kwa sababu ya "Uoga" aka kuwa Chini yake ambako wewe unadhani ni "heshima" unaendelea kuwepo humo.




Ikiwa unatoa "Heshima" huku unahasira au  Moyo/Roho inakuuma ujue hiyo sio Heshima bali ni "Uoga" ambao ukiendelea utakusababishia Matatizo ya Kiakili na Kisaikolojia(bila wewe mwenyewe kujua), utaishi kwenye Ndoa kwa sababu ya kufurahisha Jamii/Famili/Ukoo na sio kwa ajili yako na Mumeo na pengine Watoto kama mtaajiliwa.



Huenda ukawa unamalizia "machungu" yako kwa...labda Msaidizi wako,Marafiki zako au Watoto. Unaweza kuwa mwenye hasira kwa watu wengine ambao hawahusiki.....unatoa Sauti/unakuwa juu huko kwasababu huwezi kufanya hivyo kwa Mumeo. Hivyo unaumiza watu wengine wasio na hatia kwa Upumbavu wako wa kuwa Chini ya Mumeo kama sehemu ya Kumheshimu!!




Ndoa ni Muungano wa Watu Wawili, Wewe na Mumeo. Msingi wa Ndoa yenu unatakiwa kuwa-based na kuendelea kujengwa na pande zote....baadhi ya Mafunzo kutoka kwenye Imani za Dini yamepitwa na Wakati, ni vema kutumia Common Sense rather than kufuata "Mafunzo" ambayo ni Radical na zimeegemea kwenye Mfumo Dume zaidi na kutokana na Maisha yalivyo sasa ni kama vile baadhi hazileti maana? Kwamba tunakabiliana na changamoto tofauti na zile za Miaka 2000BC.




Sasa Heshima kwa Mwanaume ndio sababu kuu/pekee ambayo husababisha Wanawake waambiwe/lazimishwe kuwa Chini ya Mwanaume. Kama nilivyokusia hapo juu, Kuheshimiwa kwa Mwanaume  ni Muhimu sana kama ilivyo kwetu Wanawake kwenye kujaaliwa,kulindwa na kupendwa (kuwa cherished).



Nnachojaribu kusema hapa ni kuwa, huitaji kuwa Chini ya Mwanaume! akifanya ujinga muweke sawa ila sio kwa Kumfokea bali kuwa-firm.....kwamba aone kuwa unachosema hutanii na  hutaki mchezo...upo very serious.


Chagua Maneno ya kutumia, ikiwa unahitaji muda kufikiria, jipe muda na tafuta nafasi uwakilishe Issue inayokusumbua. Ikitokea kitu na kinahitaji mabishano basi Bishana kwa heshima bila kutoka nje ya Mstari wa Heshima na kutumia maneno machafu/kashfa..



Mara nyingi Wanaume huchukia ikiwa wewe Mwanamke unaonekana "smarter" kwenye Mambishano yenu na ili kukunyamazisha hukimbilia kutumia Kashfa au maneno machafu yatakayokuumiza hisia, sasa hata kama yeye atayatumia bado huitaji kumrudishia hapo kwa hapo. Ugomvi ukiisha/poa muelezee hisia zako za kutokupendezwa na matumizi ya maneno Machafu/Mabaya/Matusi.



Kuwa Chini ya Mtu yeyote sio rahisi, achilia mbali Mumeo, mie binafsi siwezi na sitokaa niweze na Yaye Mume wangu analijua hilo....sitaki/sipendi ujinga(naturally mie ni Mkali), nina hoji kwenye kila jambo/kila kitu ambacho kinagusa Familia yetu na hasa Watoto wetu....nadhani hii ni kutokana na sehemu ya "career" niliyopitia? sijui!!



Ndoa ni Kazi ya kila Dakika, Kila saa na Kila Siku, ukiwa mvivu basi utakimbilia "mwanamke lazma awe chini ya Mumewe"....acha Uvivu, do your Job! Kama huna Muda wa kufanyia kazi basi usifunge Ndoa....Ndoa haihitaji wavivu.


Usikose Post ijayo ya "Jinsi" ya kuonyesha Heshima kwa Mumeo. Nathamini na Kuheshimu Muda wako hapa, ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai!

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao