Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2015

Miaka 30 ndio mwisho wa kutaja Umri wako...

Kwa mwanamke.....habari za Masiku tele? Ahsante kwa kuichagua Blog hii. Nilipojuja Nchi hii miaka zaidi ya 10 nilikuwa kwenye my early 20s na nilikuwa nasafiri kama mtoto....sio nilifoji la hasha! Wakata Tiketi waligoma kukubali umri wangu na wakasema mie ni binti wa miaka 15yrs. Nilinilikuwa nakaa Kijijini halafu nasoma London) na Kiingilishi changu cha kudandia akuu mkidada wala sikubisha so nikakata Kibali cha Usafiri kama mwanafunzi wa Kimataifa wa Miaka 15 ambacho ni Chee. Enzi hizo (2000s) hakukuwa na mambo ya kufuatiliana kwenye Passport. FAST FOWARD....nikawa na Mume ambae anakunywa Pombe, nikienda nunua Pombe wanagoma kuniuzia eti mpaka niwe na Miaka 25 hihihihi. Nikiwaambia mie ni mama wa watoto 2 na nipo in my 30s wananicheka na kunambia a 23yr old woman can have a child too so wanaomba  niwaonyeshe kithibitisho cha umri(Driving License) nawaonyesha.....misamaha mingi ikijumuishwa na hongera kwa kuluku so yang'i. Au kwa maana nyingine am a 23yr old who look like a

Usafi na Kinyaa....

Ni vitu mbili tofauti....Natumai umeamka/shinda salama. Mtu kuwa msafi haina maana ana kinyaa na mwenye Kinyaa sio kwamba ni msafi pia....japokuwa wapo wasafi na wanakinyaa pia(mie).....hivi ni kinyaa au uoga wa kupata maambukizo? Nakumbuka nilipokuwa nakwenda Hospitali kwa matibabu au kumtembelea Mgonjwa....nilikuwa naumwa kichwa balaa. Nikitoka tu maeneo ya Hospitali napona. Natabia ya kubana Mkojo kwa muda mrefu(usijaribu hii ila kama ni mtu wa Kuendiketa poa) ili nisitumie vyoo vya wote(public)....Haja kubwa (sorry 4 TMI)huwa haiji nikiwa kwa watu au nje ya kwangu/kwetu.....hii sasa ni Saikoloji issue. Jana nimetoa siri yangu kwa Asali wa Moyo kuwa tukienda kwa watu(ndugu zake incl) huwa siogi wala kutumia vifaa vyao vya kujisafishia. Nitafungua Shower vema tu au kujaza Ndoo maji(inategemea nipo wapi) na kuacha shower iendelee au kumwaga maji as if naoga kumbe nanawa miguu...hihihihi. Badala ya kucheka akabaki kaduwaa hehehehehe well sina siri tena maana hata wewe msoma

Kiswahili Kigumu....spesho Post kwako!

Heyaaa. Ahsante kwa kuichagua Blog hii. Naona Idadi inaogezeka kila siku. Hi wa USA...How do you do wa hapa nilipo....jambo Afrika Mashariki.....Hello wengine wote popote mlipo Ughaibuni. Tambua kuwa ninathamini ugeni na ukazi wako wa muda mfupi au mrefu(unaposoma).....natumaini naweka makunyazi usoni kwako ama kwa kutabasamu au kwa kukunja sura. Umewahi kuamishwa(na Gugo) kutoka Kiinglishi kwenda Kiswahili halafu ukashindwa kuelewa....yaani unachanganyikiwa na hujui nini kina maanisha nini? Kwasababu ninablog kwa Kiswahili mara nyingi Gugo wananijaribu kutumia Blogger kwa Kiswahili ambayo siielewi. Mara chache nasoma Blog za Kiswahili kama vile http//www.tech255.com , www.bwaya.blogspot.com (simu haniruhusu kuweka link so yeah copy and paste uone waandikacho)na nyingine za Kuelimisha. Huko pia huwa nachanganyikiwa na kutokuelewa baadhi ya maneno ambayo nadhani ni mapya. Ila tofauti ni kuwa yapo kwenye sentensi hivyo inanirahisishia kuelewa Mwandishi alimaanisha au anamaanisha n

Vita ya Vibonge(plus size) kwenye Umodo!

Uchibonge aka Undimbo aka minyama uzembe....hello! Habari ya JumaSita? Jana nilikuwa naangalia kipindi cha Plus size War. Ambapo walizungumzia mengi kuhusiana na mwanamke kuwa mnene. Walianza na kuwasifia Bloggers wa Fashion ambao ni wanene halafu wakaenda ni nani hasa anapaswa kuwakilisha Plus sized women kwenye Umodo wa Mavazi to changamoto za wabunifu na waendesha maduka yanayouza nguo kubwa. Ila kilichonivutia zaidi ambacho nakiunga mkono kwa sababu nilikuwa najiuliza siku nyingi. Kwanini a size 14-16 anamodo kama Plus size? Well labda ni plus kwasababu UK size ndogo ya mtu mzima inayopatikana madukani ni 6 so ukiidabo au plus unapata 12 so year mie pia ni Plus size hihihihihihi. Mungu nisamehe. Binafsi nadhani Mawakala wa Plus size wanakosea.....japokiwa kwenye Documentary hii wamejielezea kwamba Soko walilonalo na demand wapatayo sio plus size tuitakayo watu wa kawaida kwamba ni size 20 to 34 au zaidi. Wanene hawana option linapokuja suala la fashion na Trend kwasababu mad

Elimisha mwanaume asibake(Rape) mwanamke....

....sio kufundisha Mwanamke jinsi ya kuzuia asibakwe! Habari ya wewe? Nasema ahsante kwa kuichagua Blog hii. Unategemea Nchi iliyoendelea kama UK kwamba huwezi kusikia suala la kuelimisha Wanaume kuhusu Ngono ili wasibake Wanawake via Media eti! Wapo wachache walioelimika na wenye kumthamini Mwanamke na kumheshimu na kutomjaji kutokana na Mavazi yake. Pia Hukumu kali dhidi ya Ubakaji inasaidia kwa mbali. Lakini bado kuna Wanawake na Wanaume ambao wanadhani kuwa Mwanamke kubakwa ni Kosa lake na hivyo kufundisha Wanawake namna ya kuzuia Kubakwa as in wasivae Mavazi yanayovutia Wanawame n.k. Mwanamke Habaki.....sasa kwanini yeye awe responsible kuji-limit kwa ajili ya Mwanaume? Kwanini Mwanaume asifunzwe kuji-control na kutomuona Mwanamke kama object ya kumalizia haja zake za Kimwili? Kanini Mwanaume asifunzwe kuwa ili kufurahia Tendo ni lazima au ni vema upande wa pili ukubali kutoa ushirikiano na sio kulazimishwa? Kwanini Mwanaume asionywe kuwa Kubaka ni Kosa? (Natambua wapo wan

Pale Gugo inapokuomba kutunza kila kitu chako...

Kuanzia Picha, Emails, Work Docs na bila kusahau details za kubanki Online. Habari ya J'pili na ahsante kwa kuichagua Blog hii. Kwa ubize wa maisha hakika utamshukuru Gugo kwa kukurahisishia......na yeye anakuukiza unataka nikumbuke pin au password yako fo yo konviniensi....na wewe unabonyeza Ok kwa hiyari kabisa. Tena inakuambia pia ni rahisi kufanya manunuzi online ukiseti Gugo loko(mahali ulipo)......na wewe unakenua na kukubali settings hehehehehe you are done Mwananchi. Baada ya miaka kupita utaanza kulalamika kwanini unaibiwa pesa au kwanini kila mtu anajua unapoishi. Ikitokea umefanya Jinai ndio utaijua Google na vitongoji vyake....siku itokee unautaka Ubunge sijui Uwaziri watu wanavuta Gugo na kupata kila kitu. Aiii nafurahia urahisi wa ku-shop online na kujua nini kinapatikana wapi lakini hayo mengine natunza na kukumbuka mwenyewe. Asante nashukuru Google. Well wanajua kila kitu cha yeyote anaewatumia isipokuwa hawawezi kuweka wazi details zako zipatikane kwa sabab

Faida ya kumchukia mtu usiemjua....

Ni nini hasa? Unajua kuna watu maisha yao ni ya huzuni sana bila wao kujijua. Anakaa kabisa na kutulia kisha anaanza kurusha maneno makali. Unawezaje kum-attack mtu kwa matusi wakati humjui? Hupendi anachokiandika au kukisema fair enough....sasa kitu gani kinakupeleka kwenye Ukurasa wake wa FB au Twitter au Blog na Sites? Binafsi kama sipendezwi na Blog fulani basi sitoitembelea tena.....muda wa kuendelea kufuatilia anachokiandika ambacho mimi sikipendi sina. Heri nitumie muda huo kupeleka Wanangu Park wakacheze au nikoshe nywele zangu au kutengeneza Kucha au kwenda kufanya manunuzi at the end nifurahi moyoni......there are so much more in life than being a Troll. Unakosa usingizi ukifikiria nini cha kwenda kumuambia mtu in an attack way kwenye Site au Page yake.....unapata faida gani? Mimi Dinah kuacha kublog Dinahicious is nothing to do with January Makamba au mabadiliko ya Sheria Tz ni uamuzi binafsi. Ngoja nikusaidie kuelewa: Google walipokuja na mabadiliko ya Sheria Mwezi w

Namba ya Simu imekuwa too personal....

Heyaaa! Unawajua wale watu wanagawa namba yako ya Simu kwa watu wengine bila idhini yako. Tangu enzi mie nachukulia namba yangu ya simu ambayo haihusiani na "Kazi" ni personal na hakuna mtu anapaswa kuwa nayo isipokuwa wale ambao nadhani ni muhimu maishani mwangu kama sio leo basi huko baadae. Sasa kutokana na Maendeleo ya Kitekinolojia Simu si ndio zimezidi kuwa PERSONAL kuliko namba? Halafu unashangaa kwanini watu wanaweka Passwords au PIN ku access simu zao. Nilipopata simu yangu Mpya (kumbuka nimekuwa nyuma na  Teknolojia ya  Simu kwa Miaka 3.5)....so niliponunua ze latest simu si ndio ikanishtua. Ile mambo ya urahisi wa kupokea na kutuma Emails mdio ikanitisha kabsaaa. Nime add Email address nikaletewa the whole thing.....kumbuka sijagusa emails via desktop kwa miaka sasa nilipoona mafolda yaliyokontaini barua za wapita njia na some picha zao dated back in 1999 to 2005 si nikapata Mini heart attack! Nikabonyeza futa daima milele. Zaidi ya hizo kuna zile unasubiri m

Jaribio.....jaribio la Picha!

Tatizo...kila nikiambatanisha Picha Post inagoma ku-publish. Nimapunguza ukubwa....nimebadilisha settings lakini Ola!  Nimeambatanisha picha kwenye post ya jana lakini haionekani....kwenye hii pia nimeweka picha. Heeeelp tafadhali. Ahsante.

The other woman kwa Kiswahili ni Kimada?

Jana nilikuwa masoma Magazine moja hivi nikakutana na stori ya mdada Mashuhuri kiasi cha kutosha Uingereza. Alikuwa akizungumzia suala la kuwa Kimada ukitumaini au kuomba kama sio kusubiri Mwanaume unaemuiba amuache mkewe na watoto wake ili mwanaume huyo awe na wewe full time. Akaongeza....Mume wa mtu alipomtokea kabla hajajua kuwa ni mume wa mtu alimkubali then Jamaa akamwambia ameachana na Mkewe na Talaka itachukua muda  kiasi hivyo sio mbaya kama wakilianzisha. Mkimama akagoma na kumwambia watatoka soon baada ya Talaka kukamilishwa kwasababu hataki kuwa sababu ya kuharibu Maisha ya Mkewe na Watoto wake. Akagusia kwa kusema....wanaume  Wazinzi huanza kukuvuta kingono via mitandao ya kijamii na kuomba uwaambie utawafanyia nini ikiwa utapata nafasi ya kuwa nao. Kisha huenda na kuponda maisha yao ya kingono na Wake zao kwako.....halafu wakiona upo interested wanaongeza "i wish my wife angekuwa open minded kama wewe"(wakati uliyomwambia ni masuala ya kawaida tu ambayo kila

Sio wote Ughaibuni tulifika kwa Ndege....

Mabaharia.....I see ya! Mambo vipi lakini(i sound like a male)? Ahsante kwa kuichagua Blog hii. Ujue huku nje ya Tanzania kila mtu anauchungu wa maisha kivyake kutokana na sababu zilizomleta....sio mnatujaji kwa kutujumuisha bana. Kuna wale walikuja kuongeza Elimu ili wakirudi waitumie ilimu yao ya kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi yao Tukufu Tanzania. Halafu wapo waliochukia maisha yao yalivyokuwa Bongo na kwa hasira kutaka kwenda kujaribu au kuanza upya huko kwingine.....hawa kurudi sio chee(as in rahisi). Wengine walipelekwa na Wazazi wao baada ya kuanza tabia mbaya na zenye kutia aibu Wadhifu....sasa ili Wazazi waendelee ku-keep Status.....er ya Uchungaji wa Kanisa, Ukuu wa Jeshi au Uwaziri n.k so unapelekwa Nje ukafanye Umalaya wako kwa nafasi. Pia kuna akina sie tulioletwa huku kama Mtaji au Urithi.....kwamba Wazazi wanatumia Akiba ya familia ili ukasome na ukimaliza na kuanza kazi ama ulipe Deni na Riba au uwasaidie Nduguzo ambao technically umetumia Mgao wao wa Urithi

Come to terms with your Uchibonge....

Hello! Naweka viraka mbinguni ujue(mekuwa busy namna hiyo). Mwisho wa wiki nilipata wasaa wa kupekua pekuwa YouTube na huko nikakutana na "how to gain weight".....nikabofya na kuanza kusikiliza hadithi moja baada ya nyingine kuhusu Wanawake wanaotaka sana kunenepa. Unajua unapomsikiliza mtu au kusoma hadithi yake na kuhisi kuwa anakysemea au kukuwakilisha wewe? Yaani anakugusa kumtima. Nikakumbuka jinsi nilivyokuwa Chikonda (skinny)enzi zile nakua(nimeacha kukua nilipofikisha miaka 25 nadhani). Story Time: Nilikuwa mwembamba kiasi kwamba baadhi ya watu walidhani nina Ugonjwa. Mmoja wa Binamu zangu alikuwa akiniambia "mtu mwenyewe maiti wewe.....umebaki mifupa tu". Nilipofika late teen baadhi ya watu Familiani wakawa wanasema ninatoa mimba sana wakati sikuwa namjua mwanaume sasa sijui Mimba ziliingia kwa Roho mtakatifu! Wengine walisema naiga Uingilishi figa na hivyo kutumia madawa ya kujikondesha. Nilichoka kusakamwa kwa uchikonda wangu ambao sikuuom

Wale akina bila "mimi" usingekuwa hapo!

Unawajua? Kwanza haujambo? Anhsante sana kwa kuichagua Blog hii. Kwa sie wa Ughaibuni (tuishio nje ya Tanzania)au wale tulioitwa Mjini kusoma au kufanya Kazi pia sisi wa Mtaani tuliamua kujaribu Fani na tukaipatia na tumefanikiwa kimtindo ndio huwa tunabeba hili limzigo. Sawa pengine bila wewe kweli asingekuwa hapo lakini ulifanyanini hasa kwenye mafanikio yake aliyonayo hivi sasa......zaidi ya kuwa njia tu ya yeye kufika hapo na actually ukajaribu kuharibu bila mafanikio? Kwa kawaida sisi wa Ughaibuni tukikaa sawa huwa tunapenda kusaidia wengine waje kujaribu maisha huku. Wanafikia kwako na unawasaidia kutafuta Kazi  na baada ya hapo nauli kwa miezi kadhaa halafu wanaanza kujitegemea. Kutokana na Ughali wa Maisha Ughaibuni well UK + "kikacha" unapaswa kuchangia sehemu ya Bills.....hakuna cha bure na hakuna "nakaa kwa Anti hapa" lipa bill dadaaa au nakutimua.....hapa sio Tanzania. Anyway.....maisha yanakuwa magumu kwa upande wako so unaongeza bidii kwenye kus

Kumfulia nguo sio wajibu ni msaada.

Heri ya Ijumaa! Najua umewahi kukutana au kusikia watu wakisema wanataka kufunga ndoa ili wapate watu wa kuwafulia nguo na kuwapikia er futari? Pia umewahi kuona wanaume wakimsifia mwanamke kwasababu akienda kwake lazima atamfulia nguo na hivyo mwanamke huyo anafaa kuwa mke au bado? Unakuta mtu anakasirika kabisa kwasababu nguo zake hazijafuliwa na kunyooshwa tayari kwa ajili yake akidhani kuwa hiyo shughuli ni wajibu au kazi ya Mpenzi wake(wanasahau kuwa kuna Dobi kila Mtaa). Kwa wale wanaofanya kazi nyumbani(mama wa nyumbani) kazi zao ni nyingi kuliko kazi yako nje ya nyumbani hivyo anapokufulia nguo ni msaada.....kwamba anakusaidia so usizoee ukadhani kuwa ni wajibu wake kukufuli. Kunyoosha Nguo aka kupiga Pasi huku Ughaibuni inachukuliwa kama kazi ngumu kwamba inaweka presha kwenye Miguu na uti wa Mgogo sasa imagine mkimama anaefua(kwa kuinamisha mgogo pia).....! Nina sifa nyingi kama mwanamke kwenye "shughuli" za nyumbani lakini sifa kuu ni kunyoosha Mashati na Sur