Skip to main content

Social Media, kama ilivyo kwa Dini ni chanzo cha Ndoa/Uhusiano wako kuyumba.


Jambo!

Siku kadhaa niliuliza "kiutani" kuwa Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume  kwa Vijana(chini ya Miaka 60)Nchini Tanzania au pengine Afrika linasababishwa na nini? Wawili watatu walidai kuwa Vijana siku hizi wanapiga Mkono(kujichua) kupitiliza, binafsi nilidhani kuwa ni Mawazo kutokana na Ukosefu wa Ajira(Kipato).


Hivi majuzi nikakutana na Majadiliano ya Vijana (huku niliko) wakijadili ni namna gani Instagram inawafanya washindwe kuwa watendaji wazuri Kitandani. Sio tu kwamba hawawezi ku-perform bali pia wakifanikiwa kuinuka basi mwenzo huwa mreeeefu na hawafikii mwisho.


Kwa kawaida(kiuzoefu) Mzunguuko wa kwanza unaenda kwa Dakika 45 bila Mwanamke kuhisi kuchoka na bila kubadilisha Mikao(unabadili movements za Kiuno/Nyonga), na hii ni kwa Mwanamke mwenye uwezo wa "kukojoa" zaidi ya  mara moja ndani ya Mzunguuko Mmoja(Hisabati nazo zinanifuata kila mahali...I don't like them huh!).


Kumbuka baada ya Mwanamke(wa kawaida, sio sie special wa Goli 3 per Mzunguuko hihihihi) kufika Kileleni(kukojoa) ataweza kukusindikiza kwa dk nyingine 20, zaidi ya hapo anaishiwa "hamu" na kuanza kukauka na hivyo kufanya Tendo kuwa karaha.


Sasa unajiuliza Insta inaingilianaje na Mwendo mrefu au kushindwa kiutendaji? Well ni rahisi tu. Mwanamke wako sio kama wale unaowaona kwenye Instagram. Huenda wewe ni mmoja kati ya wale wengi ambao Mlifunga Ndoa kwa kufuata Tabia njema/Alikuwa mbele yako/Umetafutiwa/Umri unakutupa Mkono na sio Tabia njema, Mwonekano uutako kipindi chote kabla ya Uzee na labda Akili na utayari wa kutulia(umemaliza Starehe za Ujana).


Nani anafanya mapenzi na Akili au Tabia njema? Sawa  pengine kwenu Wanaume muhimu ni kuingiza tu basi, lakini kuwa wazi na nafsi yako! Utataka kuingiza tu ikiwa huna jinsi (upo desperate) lakini ukiwa na Choice/option sidhani kama utaingiza tu popote, lazima macho yako yapendezwe, yavutike na muonekano wake.


Au kama hujaoa basi inakuuwia vigumu kuwa na Mwanamke umtakae kama wale uwaonao Instagram. Mara nyingi unatamani ungefanya nao mapenzi, lakini kutokana na umbali au viwango inakua ngumu. Lakini kwasababu ni Insta inakuwa rahisi kwako kumfuatilia/wafuatilia wachache wanaokuvutia na hata kuzungumza nao.


Ikiwa unatumia muda Mwingi na Insta(Twita na platform zingine) THOTs/Models au Wake za watu inaweza kuathiri Utendaji wako na ukajikuta unahitaji Pombe kali kama vile Jack Daniels au Konyagi, pengine Viagra za Kiasili ili kufanya Tendo vilivyo. Unaweza kudhani ni kawaida yako kupiga Pombe Kali.....lakini ukweli ni kuwa huwezi tena Kiasili kwasababu Picha uliyonayo Kichwani inayokuvutia sio huyo Kimama aliekitandani/mbele yako. Umekuwa tegemezi wa Pombe/na Dawa.


Matumzi ya Bidhaa hizo hukufanya uende mwendo mrefu kupita Kiasi, Mf Jack Daniels unaweza kuondoka hata Masaa Matatu(Kwa Wanawake ukuje next time nikuambie jinsi ya kukabiliana na mwendo mrefu huku ukifurahia) na bado usifikie Mshindo.


Hapa Mwanamke anajishtukia na kudhani kuwa hakuvutii tena kwasababu siku hizi hauji haraka kama zamani, yaani madoidoe yake yote yanapita bureee hata lile Bao la kwanza  baada ya Siku tatu bila Tendo linachukua Nusu saa kuja. Anaanza kukuhisi vibaya, anahoji, analaumu n.k.


Wewe (Mwanaume) pia unaweza kudhani kuwa Mpenzi wako hakuridhishi tena na hajui, kajisahau au unaanza kupoteza Uanaume wako na hivyo kujaribu mwingine nje ya Uhusiano uone tofauti....yeah kuna mijamaa mijinga that much. Badala ya kutafuta suluhu na kubadilisha inaenda kuongeza tatizo. Na huo ndio mwamnzo wa kuyumba kwa Ndoa/Uhusiano wako.


Dini inayumbisha Ndoa/Uhusiano? weeee! Usikose Wiki ijayo.

Kwasasa tambua kwamba nathamini Muda wako hapa na Shukrani kwa Ushirikiano.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao